• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 1:47 PM
Sita wafa katika ajali

Sita wafa katika ajali

Na SAMUEL BAYA

WATU sita walifariki Jumamosi katika ajali iliyotokea kwenye barabara kuu ya Nakuru-Kericho.

Kulingana na maafisa wa polisi pamoja na wahudumu wa hospitali ya Kericho, watu watano walifariki papo hapo huku mmoja akiaga dunia alipokuwa akitibiwa katika hospitali kuu ya mjini Kericho.

Kulingana na msimamizi wa polisi eneo la Londiani, Bw Musa Kongoli, ajali hiyo ilitokea baada ya trela lililokuwa likitoka Nakuru kupoteza mwelekeo na kugonga magari mengine.

“Ajali hiyo ilihusisha trela ambalo lilikuwa likiekelea upande wa Kericho kutoka Nakuru. Dereva wa trela alipoteza udhibiti alipofika eneo hilo na kugonga magari mengine matano ambayo yalikuwa ni pamoja na matatu mbili. Watu watano, wanaume watatu na wanawake wawili walifariki papo hapo,” akaeleza Bw Kongoli.

Wa sita alifariki akipokea matibabu.

Aliambia wanahabari kwamba walioaga dunia walikuwa katika matatu iliyokuwa ikielekea Nakuru kutokea Kericho. Dereva wa trela alipata majeraha na anaendelea na matibabu katika hospitali hiyo kuu ya Kericho.

You can share this post!

Bayern wazidi kufuka moto Bundesliga

Mario Gotze kuagana rasmi na Dortmund mwishoni mwa msimu huu

adminleo