• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:55 AM
Waiguru akataa kuidhinisha fedha za ziada kwa bajeti ya corona

Waiguru akataa kuidhinisha fedha za ziada kwa bajeti ya corona

NA GEORGE MUNENE

Gavana wa Kaunti ya Kirinyanga Ann Wainguru amekataa kuidhinisha mabadiliko yaliyowekwa kwenye bajeti ya kukabiliana na janga la corona na madiwani wa kaunti hiyo.

Bi Waiguru aliwalaumu madiwani hao kwa kupenedekeza mabadiliko yatakayowaumiza walipa ushuru wa kaunti hiyo.

Gavana huyo alisema kwamba bajeti hiyo ilipaswa kuwa ya Sh20 milioni na ilifaa kufadhili mikakati ya  kupunguza kusambaa kwa Covid-19.

Badala yake madiwani hao walipendekeza bajeti ya Sh100 milioni ambayo awali ilikuwa imetengewa hospitali ya Kerugoya na Sh30 milioni zilizotengewa mafuta na miradi ya wadi.

“Tulikuwa tumetenga pesa za kupambana na janga la corona lakini sasa madiwani wamekekuwa kikwazo kwa kuanzisha mabadiliko ili wajitengee pesa zaidi ,’’alisema Waiguru.

You can share this post!

Zoom inavyotumika Meru kuwafaa wasiojiweza

Waandishi wa Afrika walaani mauaji ya George Floyd

adminleo