• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Seneta Cherargei ahusika katika ajali ya barabarani

Seneta Cherargei ahusika katika ajali ya barabarani

Na CHARLES WASONGA

SENETA wa Nandi Samson Cherargei anapokea matibabu katika hospitali ya kibinafsi ya St Luke, Eldoret baada ya kuhusika katika ajali ya barabarani Jumamosi asubuhi.

Duru zinasema kuwa ajali hiyo ilitokea katika barabara ya Eldoret kwenda Kapsabet katika eneo la Kapseret.

Bw Cheragei aliripotiwa kupata majeraha madogo kufuatia ajali hiyo.

Picha za gari aina ya Prado, linaloaminiwa kuwa lake Seneta Cherargei, lililobondeka zilisambaa kwenye mitandao dakika chache baada ya ajali hiyo.

Bw Cherargei ni miongoni mwa viongozi wa jamii ya Wakalenjin walioandamana na Naibu Rais William Ruto katika mkutano wa kisiri katika eneo bunge la Chesumei nyumbani kwa mzee mmoja wa ukoo wa Talai, uliosemekana na kumtakia “heri njema” katika azma yake (Ruto) ya kuingia Ikulu 2022.

Katika mkutano huo wa faragha Dkt Ruto aliripotiwa kukutana na zaidi ya viongozi 50 wa jamii ya Nandi, wakiwemo wazee na viongozi wa kidini.

Wakenya mitandaoni wamemtakia Bw Cherargei afueni ya haraka.

You can share this post!

ODM yatarajia BBI kutia nguvu ‘risasi’ ya Raila

Amdunga kisu mumewe mara 11 wakizozania kuosha vyombo

adminleo