• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 6:55 PM
Ng’ombe 24 wa mbunge wafa baada ya kula chakula hatari

Ng’ombe 24 wa mbunge wafa baada ya kula chakula hatari

NA GEORGE SAYAGIE

Mbunge wa Emurua-Dikir Johanna Ngeno anakadiria hasara baada ya ng’ombe wake wapatao 24 aina ya Holstein Friesian wenye thamani ya Sh2.5 milioni kufa baada ya kula chakula kilichoangizwa kutoka nchi za nje.

Mbunge huyo wa Kanu ametishia kushtaki wauzaji wa lishe hiyo akisema kwamba ng’ombe hao walikuwa wanatoa maziwa lita 40 kila siku.

“Nilienda kwenye maabara ya kitaifa ya dawa na sampuli hizo ili kuchunguza kilochopeleka kifo cha ng’ombe wangu lakini hii lazima niende kortini,” alisema Bw Ngeno.

Katika mazungumzo ya simu na Taifa Leo Jumamosi, mbunge huyo alisema kwamba ng’ombe hao walianza kuanguka mmoja baada ya mwingine baada ya kula chakula hicho.

Kulingana na Bw Ng’eno, chakula hicho hatari kinapatikana kwenye maduka ya kuuza chakula cha mifungo.

Maelezo yaliyochapishwa kwenye magunia hayo yanaonyesha kwamba ni chakula cha mifugo, lakini tarehe ya chakula hicho kuharibika ni Januari 28, 2020.

You can share this post!

Watu 6 wajeruhiwa katika ajali ya ndege Meru

Waombolezaji 25 kutoka Mombasa wazuiliwa Siaya

adminleo