• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Jinsi ya kusonga ugali

Jinsi ya kusonga ugali

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 5

Mudda wa mapishi: Dakika 20

Walaji: 3

Vinanyohitajika

• maji vikombe 3

• unga wa ugali

• sufuria

• ubanio

• mwiko

• jiko la aina yoyote ama mkaa, umeme au gesi

Maelekezo

Injika sufuria yako mekoni ikiwa na maji yenye unga kidogo.

Hakikisha maji utayoweka yatakutosha. Pia hakikisha moto unakua sio mwingi bali ni wa wastani.

Pale maji yatakapochemka na kutokota, weka unga kiasi kwenye maji hayo huku ukianza kuusonga taratiiibu na ubanio.

Songa ni kama unauminya huku unauzungusha kwa mwiko. Utaona mabadiliko ule uji utakuwa mgumu kila unapoendelea kuusonga.

Ukishaona mabadiliko hayo, punguza moto na ufunike ugali wako kwa dakika 10.

Andaa sahani au hotpot kisha uepue ugali wako.

Pakua kuliwa na mboga yoyote ile uliyoiandaa; inaweza ikawa samaki, nyama au chochote ukipendacho.

Mboga sukumawiki ba mayai. Picha/ Margaret Maina

You can share this post!

Ruto akwepa kuandamana na Uhuru tena

Namna ya kujitengenezea sosi ya nyanya nyumbani (tomato...

adminleo