• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 11:38 AM
Jombi ageuzwa gumzo mtaani kwa kuoa ajuza

Jombi ageuzwa gumzo mtaani kwa kuoa ajuza

Na JOHN MUSYOKI

KIVANDINI, MATUU

KULIWA na kioja hapa mzee mmoja alipozomea mwanawe kwa kuoa mwanamke aliyemzidi umri.

Inasemekana jamaa alikuwa kapera kwa muda mrefu lakini alipoamua kuoa, alishangaza watu  kwa kuoa mwanamke mzee kumliko hadi akawa ngumzo kijijini.

“Jamaa alioa mwanamke mzee sana hadi watu wakawa wanamsema jambo ambalo halikumfurahisha baba yake.

Siku ya kioja, baba ya jamaa alipogundua kuwa watu walikuwa wakimkejeli mwanawe kwa kuoa mwanamke mzee, alienda kwa mwananawe na kuanza kumkemea.

“Nimepata habari kuwa eti mwanamke uliyemuoa majuzi ni mzee kukuliko.

Kwa nini ulioa mwanamke mzee na kuna mabinti wa umri mdogo na wabichi wa kuchumbia?

Una akili timamu ama ulirushiwa ndumba na mwanamke huyo? Watu kijijini wanakusema kila kuchao kuwa haukufanya vizuri kuoa mwanamke huyu mzee,” baba ya polo alilalamika.

Alimtaka kumtimua mwanamke huyo na kutafuta mwingine wa kuoa ikiwa alitaka baraka zake za kuanzisha familia.

Hata hivyo, jamaa alikanusha madai ya babake ya kumtaka amfukuze mkewe kwa sababu alikuwa  mzee kumliko.

“Wacha wanaosema waseme. Watasema mchana lakini usiku watalala. Kinachowawasha ni kipi? Hata kama nilioa mwanamke mzee kuniliko, shida yao ni gani?

Ndio nilioa mwanamke mzee lakini hawana nafasi ya kukatiza mapenzi yetu kwa kusema au wewe kuja kunizomea kama mtoto.

Hata kama mke wangu ni mzee nilimchagua kwa sababu nilimpenda. Hakuna  aliye na haki ya kuingilia ndoa yangu na sitakubali upuzi huo,” kalameni alisema.

Ilibidi buda kuuma kona kalameni aliposhikilia msimamo wake na kukataa kumfukuza mkewe.

Alimweleza mzee kutokanyaga kwake kujadili mkewe. Hata hivyo haikujulikana iwapo ndoa yao ilidumu baada ya mzee kukosa kuwapa baraka.

…WAZO BONZO…

You can share this post!

Ligi ya Super 8 yashika kasi

Mwili wa mwanamke aliyetoweka wapatwa umezikwa shambani

adminleo