• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 7:55 AM
LISHE: Njegere, umuhimu mwilini na jinsi ya kuandaa

LISHE: Njegere, umuhimu mwilini na jinsi ya kuandaa

Na MARGARET MAINA

[email protected]

NJEGERE huwa na virutubisho na nyuzinyuzi. Njegere huwa na vitamini kama vitamini A, K na C ambazo husaidia katika uboreshaji wa macho, na pia damu kutotoka kwa wingi au kuganda haraka upatapo jeraha.

Pia njegere huwa na madini mengi. Madini haya hufanya kazi nyingi mwilini kama kuongeza kinga thabiti na kufanya mifupa na ngozi kuwa imara.

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Muda wa mapishi: Dakika 20

Walaji: 4

Vinavyohitajika

  • njegere 1
  • nyanya 3
  • nyanya ya kopo vijiko 2 vya chai
  • chumvi kiasi
  • mafuta ya kupikia vijiko 2
  • kitunguu maji
Njegere. Picha/ Margaret Maina

 

Maelekezo

Chemsha njegere kwa maji yenye chumvi hadi ziive na kukauka maji.

Chukua sufuria nyingine tia mafuta yakiwa moto halafu weka kitunguu kisha kaanga hadi viive. Sasa weka nyanya. Zikiiva tia njegere na ukaange kiasi; baadaye weka nyanya ya kopo.

Baada ya hapo njegere zako zitakuwa tayari kwa mlo wako. Unaweza kula kwa wali au chapati. Inategemea unapendelea kula na nini.

You can share this post!

Huduma za M-Pesa kuzimwa kwa saa 12

Sakaja alala kituoni baada ya kukamatwa katika baa wakati...

adminleo