• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:40 AM
Akanusha shtaka kwamba aliiba kuku 152 wenye thamani ya Sh53,200

Akanusha shtaka kwamba aliiba kuku 152 wenye thamani ya Sh53,200

Na RICHARD MUNGUTI

MWANAMUME anayeuza bidhaa za rejareja katika soko la Muthurwa, Nairobi alishtakiwa kumpora mwanamke kuku 152 wenye thamani ya Sh53,200.

Michael Muia Kamande alikanusha shtaka hilo la kupokea bidhaa akijifanya anaweza kuzilipia.

Shtaka lilisema mnamo Agosti 8 2020 katika soko la Muthurwa akiwa na nia ya kulaghai alipokea kuku wapatao 152 kutoka kwa Bi Margaret Wangui Thige.

Bw Kamande alidaiwa alimweleza Wangui atawanunua kuku hao wa kienyeji kwa Sh53,200.

Kiongozi wa mashtaka Bw George Obiri alieleza mahakama baada ya mshtakiwa kupokea kuku hao alitoroka hadi alipokamatwa Jumatano.

Mshtakiwa aliyekuwa na majeraha usoni aliomba hakimu amwachilie kwa dhamana.

Kiongozi wa mashtaka Bw George Obiri hakupinga mshtakiwa akichiliwa kwa dhamana.

Hakimu alimwamuru mshtakiwa alipe dhamana ya Sh100,000 na mdhamini mmoja wa kiasi hicho ama alipe pesa taslimu Sh50,000.

Kesi itatajwa Agosti 31, 2020, kutengewa siku ya kusikizwa.

You can share this post!

Beki Samuel Umtiti augua Covid-19

UEFA yatoza PSG faini ya Sh3.7 milioni kwa kujikokota...