• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Maafisa wakuu wa Chase Bank washtakiwa kuiba mamilioni

Maafisa wakuu wa Chase Bank washtakiwa kuiba mamilioni

Na RICHARD MUNGUTI

MAAFISA wakuu wa benki ya Chase Bank  (CB) iliyofilisika walishtakiwa Jumatano kwa kufanya njama za kuibia benki hiyo Sh577 milioni.

Aliyekuwa Mkurugenzi mkuu wa Benki hiyo Mohammed Zafrulla na maafisa wengine wa CB  Mabw Duncan Kabui Gichu, James Mwaura Mwenja na Makarios Omondi Agumbi walishtakiwa mbele ya hakimu mwandamizi katika mahakama ya Milimani Bi Martha Mutuku.

Washukiwa hao walikabiliwa na shtaka lingine la usafishaji wa pesa.

Washtakiwa pia walidaiwa walikuwa wanajipa mikopo bila dhamana.

Yadaiwa walitekeleza uhalifu huo kati ya Septemba 2014 na Machi 31, 2015.

Zafrulla Khan , mkurugenzi wa benki hiyo alishtakiwa kuipa kampuni ya Emmar Properties mkopo wa $ 5,475,801.92 kutoka kwa benki ya CB bila idhini.

You can share this post!

Waliotajwa kwa sakata ya NYS wajiuzulu wasitatize uchunguzi...

Kasisi akanusha kughushi hati kumiliki hospitali

adminleo