• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
LISHE: Ndizi

LISHE: Ndizi

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Muda wa kupika: Dakika 30

Walaji: 2

Vinavyohitajika

  • ndizi mbivu
  • nyama kilo 1 (iliyopikwa)
  • vitunguu maji 2
  • giligilani kijiko 1
  • Garam masala kijiko 1
  • nazi 1
  • nyanya 4 zilizoiva
  • kitunguu saumu 1
  • nyanya ya kopo kijiko 1
  • tangawizi
  • chumvi
  • karoti 1
  • pilipili mboga 1
  • Curry powder kijiko 1

Maelekezo

Kwenye sufuria mekoni, weka mafuta ya kupikia.

Mafuta yakiwa tayari, weka vitunguu maji kisha pika kwa muda wa dakika mbili.

Weka kitunguu saumu, tangawizi, garam masala, giligilani na curry powder; pika kwa dakika moja kisha weka nyanya.

Pika nyanya ziive mpaka zitengane na mafuta, kisha weka nyanya ya kopo iache kwa dakika moja.

Weka ndizi, chumvi na nyama pika kwa dakika 10 kwa moto ya wastani mpaka nyanya zichanganyike na ndizi.

Weka tui ya nazi pika kwa dakika 5, kisha weka tui zito acha mpaka tui lipungue, katia pilipili hoho na karoti pika kwa dakika 10.

Pakua na chochote ukipendacho.

You can share this post!

USHAURI: Ingawa wataalamu wanashauri watu kutonyoa nywele...

Raila na Ruto wataifaa Kenya?