• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 8:12 PM
SIHA NA LISHE: Vyakula unavyotakiwa kula kwa tahadhari au kuviepuka ili kulinda afya yako

SIHA NA LISHE: Vyakula unavyotakiwa kula kwa tahadhari au kuviepuka ili kulinda afya yako

Na MARGARET MAINA

[email protected]

MWONEKANO na afya ya mwili na akili hujengwa na chakula tunachokila.

Madhara ya chakula tunachotumia ni kama vile kuzeesha ngozi kwa haraka na hivyo hatuna budi kuvijua na kuviepuka baadhi ya vyakula hivyo.

Vyakula hivi japo tunavipenda sana lakini vina athari mbaya kwa miili yetu na muhimu kujifunza tabia ya kuviacha katika milo yetu.

Kama si rahisi kuacha kabisa basi angalau kupunguza matumizi yake.

Nyama Nyekundu

Nyama hasa nyama nyekundu ni miongoni mwa vyakula vinavyozeesha ngozi.

Nyama nyekundu inayotokana na wanyama kama ng’ombe, mbuzi, kondoo Na kadhalika ni mbaya kwa afya njema ya binadamu na hivyo kwa ngozi pia. Nyama nyekundu ina kemikali aina ya carnitine ambayo inafanya mishipa ya damu kukakamaa na kusababisha kuzeeka kwa ngozi.

Chumvi

Chumvi hasa yenye madini ya iodine ni mbaya sana kwa afya ya ngozi. Inasababisha chembechembe za nyama katika ngozi kuvimba.

Sukari

Sukari japo tunaipenda sana ni adui mkubwa wa afya ya binadamu. Inadhoofisha mfumo wa kinga za mwili. Kiasi kingi cha sukari mwilini kinafanya ngozi kuwa kavu na kufanya mwili utengeneze makunyazi kwa sababu inaharibu kemikali ya collagen na elastin ambazo zinafanya kazi ya matengenezo ya ngozi kwa kuifanya isiharibike na kuwa chakavu.

Sukari nyingi inasababisha mwili kukosa nguvu ya kupambana na bakteria. Ongezeko la bakteria hawa kunafanya utengenezwaji wa kemikali mbaya ambazo husababisha uchakavu wa ngozi.

Watu wanashauriwa kutumia sukari asilia kama ya matunda na asali kuliko zile zinazopatikana katika vinywaji kama soda,biskuti au vitafunwa vingine vyenye sukari ya kuongeza.

Vyakula vya Kukaangwa

Vyakula vya kukaangwa kama chips,nyama za kukaanga vinasababisha uingizaji wa mafuta mengi mwilini. Mafuta haya yana “Free Radicals” yanayosababisha uzibaji wa vijitundu katika ngozi. mafuta mengi mwilini yanasababisha madhara mengi mengine yakiwemo magonjwa ya moyo na kisukari.

Mkate Mweupe,Tambi na Keki

Vyakula hivi vina kemikali ya glucemic kwa kiwango kikubwa ambayo inaleta madhara ya maradhi ya ya ngozi.

Pombe

Unywaji wa pombe unasababisha kupoteza maji mengi mwilini kwa njia ya mkojo na huleta madhara mabaya kwa ngozi kwa kuifanya iwe kavu.

 Kahawa (Caffeine)

Kemikali ya caffeine iliyomo katika kahawa na vinywaji vingine inasababisha ukosefu wa maji ya kutosha katika ngozi na kuifanya iwe kavu. Lakini pia caffeine inasababisha utengenezwaji wa kemikali ya cortisol ambayo inachangia uzeekaji wa ngozi.

You can share this post!

Spurs wadhalilisha Man-United kwa kichapo cha 6-1 katika...

EAC sasa yaungana kumuunga mkono Amina Mohamed kuwa kinara...