• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 10:55 AM
Ngilu kusambaza barakoa bila malipo kwa wanafunzi 72,000

Ngilu kusambaza barakoa bila malipo kwa wanafunzi 72,000

Na KITAVI MUTUA

WANAFUNZI 72,000 katika Kaunti ya Kitui watanufaika na barakoa za bure kutoka kwa serikali ya kaunti.

Gavana Charity Ngilu jana alitangaza kuwa, wanafunzi wa Gredi 4, Darasa la Nane na Kidato cha Nne kutoka shule zote 1,400 za msingi na sekondari watapewa barakoa.

Bi Ngilu alisema barakoa hizo zilizotengenezwa na kiwanda cha nguo cha Kitui (Kicotec), zitaanza kusambazwa kesho.

“Serikali ya kaunti imetenga barakoa 200,000 na kila mwanafunzi atapewa mbili,” akasema Bi Ngilu.

Alizungumza hayo katika kiwanda cha Kicotec baada ya kufanya kikao na washikadau wa elimu kujadili jinsi ya kusambaza barakoa hizo. Mkutano huo ulihudhuriwa na maafisa wa wizara ya elimu, viongozi wa vyama vya walimu na wawakilishi kutoka chama cha wakuu wa shule.

Katibu wa Chama cha Walimu wa Shule za Upili na vyuo (Kuppet) tawi la Kitui Benjamin Mutia alisema hatua hiyo ya Gavana Ngilu ni afueni kwa wazazi.

 

You can share this post!

Tunaheshimu Seneti, Matiang’i atoa hakikisho

IG atetea polisi wavunjao mikutano ya kisiasa