• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 1:13 PM
Joho apata pigo huku wengi wakimuomboleza Hatimy

Joho apata pigo huku wengi wakimuomboleza Hatimy

MOHAMED AHMED Na MISHI GONGO

KIFO cha aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha ODM na diwani maalum wa Mombasa, Bw Mohammed Hatimy, kimeacha pengo kubwa katika serikali ya Gavana Hassan Joho.

Bw Joho binafsi alikiri kwamba kifo cha Bw Hitamy ni pigo kwake na Mombasa kwa jumla. “Mombasa imepoteza mwana wake wa kutegemewa ambaye nilikuwa namthamini sana,” Bw Joho alisema kwenye rambirambi zake.

Bw Hatimy alifariki Jumamosi akiwa katika hospitali ya Mombasa ambapo alipelekwa baada ya kupatikana kuambukiwa virusi vya corona.Bw Hatimy ambaye alizikwa jana katika makaburi ya Kikowani, alifariki siku chache tu baada ya mavyaa wake ambaye pia aliripotiwa kufariki baada ya kuugua corona.

Familia yake ilieleza kuwa alifariki Ijumaa saa tisa usiku. Wengi walimsifia Bw Hatimy wakisema hakuwa kama diwani wa kawaida na kwamba aliheshimiwa na kupendwa na wengi.

Kuanzia mwanzo wa serikali ya Bw Joho mwaka 2013, Bw Hatimy ameshikilia wadhfa wa mwenyekiti wa kamati ya fedha katika bunge la kaunti hiyo tangu Bw Joho aliposhinda ugavana 2013.

Bw Hatimy pia alitambulika wakati alipokuwa kwenye usimamizi wa michezo.Jana, viongozi wa chama cha ODM wakiongozwa na kinara wao, Bw Raila Odinga waliomboleza kifo chake na kumtaja kuwa kiongozi aliyejitolea katika utumishi wake.

“Nimezipokea taarifa za kufariki kwa mwenyekiti wa muda mrefu wa ODM tawi la Mombasa Mohammed Hatimy. Alikuwa kiongozi shupavu aliyejitolea katika kila pembe aliyoshikilia. Mungu aipe familia yake subira wakati huu mgumu,” akasema Bw Odinga kupitia mtandao wake wa kijamii.

Gavana Joho alisema kuwa Mombasa imepoteza mmoja wa watu muhimu a kutegemewa.“Kama diwani maalum alihudumu kwa kujitolea na alionyesha matunda ya kazi yake na majukumu aliyokuwa amepewa. Kwa niaba ya watu wa Mombasa natoa rambirambi zangu kwa familia. Mungu awape subira wakati huu wa huzuni,” akasema.

You can share this post!

Sharp Boys walenga kuwasha moto ligi ya KYSD 

Mpango wa kuondoa matatu jijini utakamilika hivi karibuni...