• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 6:55 PM
Ndani miaka 105 kwa kulawiti wavulana watatu

Ndani miaka 105 kwa kulawiti wavulana watatu

Na CHARLES WANYORO

MWANAMUME mwenye umri wa miaka 36 Jumatano alifungwa jela miaka 105 kwa kuwalawiti wavulana watatu kwa siku tatu mfululizo katika kijiji cha Makengi, Kaunti ya Embu.

Hakimu Mkuu Mkazi, Vincent Nyakundi alimhukumu Paul Muriithi Karuga kifungo cha miaka 35 jela kwa mashtaka matatu yaliyomkabili. Kwa jumula, Muriithi anafaa kuishi jela miaka 105 lakini mahakama ikaamua hukumu zote zitatumika wakati mmoja.

Muriithi alishtakiwa kwamba kwa siku tatu mfululizo kati ya Mei 20 na Mei 22 2017 katika kijiji cha Kanjau, Makengi, Kaunti ya Embu, kwa makusudi na kinyume cha sheria, aliwalawiti wavulana watatu waliokuwa na umri wa kati ya miaka 9 na 12.

Alikabiliwa na mashtaka matatu mbadala ya kushirikisha wavulana hao katika kitendo cha aibu.

Mahakama iliambiwa kwamba siku ya kwanza, mshtakiwa alimuotea mvulana wa kwanza akitoka kanisani na kumtaka washiriki mapenzi lakini akatoroka. Alimkimbiza mtoto huyo na kumkamata kisha akampeleka kichakani akamlawiti.

Siku iliyofuata, Muriithi aliwavamia ndugu wawili waliokuwa wametumwa dukani na nyanya yao jioni, akawanyang’anya tochi na mmoja alipotoroka, alimshika mwenzake na kumlawiti.

Siku iliyofuata alikutana na mwathiriwa wa tatu ambaye alikuwa akienda dukani na akamwambia apande kwenye mkokoteni wake uliokuwa ukivutwa na fahali amsindikize kisha akampeleka kichakani na kumlawiti.

Wavulana hao waliwaeleza wazazi wao ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Manyatta na Muriithi akakamatwa na kufunguliwa mashtaka.

You can share this post!

ATHARI ZA UFISADI: Wakenya wanavyoangamia kwa kuuziwa...

Ziara za Ruto si tisho kwa ODM – Raila

adminleo