• Nairobi
  • Last Updated April 26th, 2024 12:04 PM
Pigo kwa Kamau korti kuamuru Kesi dhidi yake iendelee

Pigo kwa Kamau korti kuamuru Kesi dhidi yake iendelee

Na RICHARD MUNGUTI

ALIYEKUWA Waziri wa Uchukuzi Bw Michael Kamau alipata pigo kubwa Ijumaa baada ya Mahakama ya rufaa kutupilia mbali ombi lake ya kuzuia akishtakiwa upya kwa matumizi mabaya ya mamlaka yaliyopelekea Serikali kupoteza zaidi ya Sh33milioni za mradi wa barabara miaka kumi iliyopita.

Majaji Majaji Mohammed Warsame, William Ouko na Kathurima M’Inoti waliakataa kumzima Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DDP) Noordin Haji akimfungulia mashtaka upya Bw Kamau.

Majaji hao walisema kesi ya kwanza dhidi ya Bw Kamau halikutupwa mbali iliondolewa baada ya ripoti kuwa aliposhtakiwa tume ya kupambana na ufisadi nchini (EACC) haikuwa na makamishna inavyotakiwa kisheria.

Bw Kamau alishikwa na kushtakiwa baada ya Rais Uhuru Kenyatta alipohutubia bunge mnamo Mei 26 2015 na kusema kulikuwa na watumishi wa umma 175 waliohusika na ufisadi wakiwamo mawaziri watano miongoni mwao Bw Kamau.

Majaji Warsame , Ouko na M’Inoti walifahamishwa wakati huo EACC haikuwa na makamishna.

Walikuwa wamejiuzulu wakiongozwa na mwenyekiti wao Bw Mumo Matemu.

Bw Kamau alisema haki zake zilikiukwa aliposhtakiwa wakati wa kwanza na hata sasa alidai DPP hakuwa na mamlaka kisheria kufufua kesi iliyokuwa imeondolewa.

Katika uamuzi wao majajaji hao walisema kuwa “ Bw Kamau hakuwa ameponyoka kabisa makali ya sheria.Hii korti imechambua ushahidi wote aliowasilishwa Bw Kamau na kufikia suluhu kuwa kesi ya awali dhidi yake haikuwa imetamatishwa mbali ilikuwa imeondolewa tu na inaweza fufuliwa wakati wowote baada ya EACC kupata makamishna.”

Korti iliamuru kesi iliyowasilishwa upya dhidi ya Bw Kamau iendelee kusikizwa na kuamuliwa katika mahakama ya kusikiza kesi za ufisadi.

Majaji Warsame , Ouko na M’Inoti,” aliyeshtakiwa pamoja na wahandisi wawili kwa kubadili ramani ya ujenzi wa barabara ya Kamukuywa-Kaptana-Kapsokwony-Sirisia mwaka wa 2008 katika kaunti ya Bungoma.

Kutupwa kwa kesi hiyo sasa kumeipa afisi ya DPP kuwasilisha ushahidi mbele ya hakimu mwandamizi Bw Lawrence Mugambi aliyesitisha kusikizwa kwa kesi hiyo asubiri uamuzi wa Mahakama ya Rufaa.

Wakili wa Serikali Bw Ashimoshi Shitambashi alipinga ombi la Bw Kamau katika mahakama ya rufaa akisema kushtakiwa kwa waziri huyo wa zamani hakukaidi haki zake.

Katika kesi hiyo Bw Kamau alikuwa ameshtaki DPP , mkurugenzi wa uchunguzi wa jinai (DCI) na EACC akisema wamekandamiza haki zake kuamuru afunguliwe mashtaka upya ilhali alikuwa ameachiliwa huru na korti hii ya pili kwa ukuu.

“Naomba hii mahakama itetee haki zangu sisihujumiwe na EACC iliyoamuru nishtakiwe tena baada ya mashtaka dhidi yangu ya kwanza kutupiliwa mbali na hii mahakama,” majaji hao walifahamishwa na wakili wa Bw Kamau.

Ameshtakiwa kubadili barabara Kamukuywa-Kaptana-Kapsokwony-Sirisia mwaka wa 2008 katika kaunti ya Bungoma.

You can share this post!

SAKATA YA NYS: Dhamana ya Lillian Omollo yakubaliwa,aondoka...

DASH 100 Bombardier: FlySax yarejelea safari zake Kitale

adminleo