• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 7:55 AM
Kenya yalima Namibia kutinga nusu fainali magongo

Kenya yalima Namibia kutinga nusu fainali magongo

Na GEOFFREY ANENE

TIMU ya taifa ya Kenya ya wavulana imetinga nusu-fainali ya mashindano ya chipukizi ya magongo ya Afrika jijini Algiers nchini Algeria, Julai 23, 2018.

Kenya ilijikatia tiketi baada ya kushangaza Namibia kwa mabao 3-1. Haikuwa imeshinda mechi katika awamu ya makundi ilipolizwa 2-1 na Nigeria na kupokea kichapo sawa na hicho kutoka kwa Zambia katika Kundi B.

Wakenya watapambana na mshindi kati ya Zambia na Algeria katika nusu-fainali nayo Nigeria ina kibarua kigumu dhidi ya Afrika Kusini.

Namibia ilikamilisha Kundi A katika nafasi ya pili kwa alama sita ilizopata kwa kunyuka Zimbabwe 5-2 na Algeria 4-1. Ilikuwa imechabangwa 4-0 na Afrika Kusini katika mechi ya ufunguzi Julai 19.

Nigeria ilipepeta Zimbabwe 1-0 katika robo-fainali ya kwanza Jumatatu. Mechi nyingine ya robo-fainali itakutanisha Zambia na Algeria. Afrika Kusini ilinyuka Zimbabwe 6-0, Namibia 5-0 na Algeria 9-0 katika mechi za makundi. Kenya haishiriki magongo ya wasichana ambayo yamevutia Afrika Kusini, Ghana, Zimbabwe, Namibia, Nigeria na Algeria.

Mashindano ya magongo yatakamilika Julai 26. Algeria inaandaa makala ya tatu ya mashindano ya chipukizi yanayojumuisha fani 31. Yalianza Julai 18. Yatakamilika Julai 28. Riadha, ambayo Kenya inasubiri sana, itaanza Machi 24.

  • Tags

You can share this post!

Crested Cranes wapata dawa yao Cecafa

Nitamwonyesha Ruto kivumbi 2022 – Joho

adminleo