• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 8:50 AM
Msigawanyike, Kalonzo ataachiwa urais na Uhuru Kenyatta – Mbunge

Msigawanyike, Kalonzo ataachiwa urais na Uhuru Kenyatta – Mbunge

Na Gastone Valusi

MBUNGE wa Kathiani Robert Mbui ameiomba jamii ya Akamba kuwapuuzilia mbali viongozi ambao wanatumiwa na wanasiasa kutoka nje kusambaratisha juhudi za kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka kuwania urais mnamo 2022.

Bw Mbui alisema jamii hiyo inapaswa kujihadhari dhidi ya wale wanaolenga kuyumbisha juhudi za Bw Musyoka kumrithi Rais Uhuru Kenyatta.

Alisema baadhi ya wabunge ambao si wanachama wa chama hicho wanatumika kuigawanya jamii hiyo.

Alisema viongozi wa sehemu hiyo wamegawanyika kwa muda mrefu.

Alitoa kauli hiyo Jumatatu katika eneo la Kathiani, kwenye mkutano na wazee.

 

You can share this post!

Mtoto aliyenusurika mafuriko kimiujiza afadhiliwa masomo

Mbunge akemea wanaohoji ziara za rais kwa Mzee Moi

adminleo