• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 8:50 AM
Kalameni amtoroka slay queen akihofia hasara zaidi

Kalameni amtoroka slay queen akihofia hasara zaidi

Na DENNIS SINYO

LESSOS, ELDORET

POLO mmoja mtaani hapa alimhepa kipusa alipoitisha pombe badala ya soda wakiwa katika eneo moja la burudani.

Yasemekana ilikuwa mara ya kwanza wawili hao kukutana ana kwa ana kujivinjari baada ya kufahamiana kwenye mtandao.

Kulingana na mdokezi, jamaa na kidosho huyo waliingia kwenye hoteli moja ya kifahari na kisha wakaitisha menu.

Licha ya jamaa kuitisha chupa ya juisi, mwanadada huyo alimwambia weita amletee chupa ya mvinyo kali.

Jamaa huyo ambaye ameokoka, alishangaa sana na kudhania kwamba huenda demu alikuwa akifanya mzaha tu.

Huku wakipiga gumzo, jamaa huyo aliletewa sharubati na kipusa akaletewa chupa ya mvinyo alioagiza.

Kulinga na mdokezi, jamaa alisema mvinyo alioagiza demu ni wa bei ghali na hutumiwa na mabwenyenye.

Binti alifungua chupa na kuanza kumimina mvinyo kwa ustaarabu huku jamaa akimtazama.

Inasemekana hamu ya jamaa kunywa sharubati iliisha. Baada ya dakika chache, mwanadada alilewa na kuropokwa huku akimpapasa jamaa kwenye mikono na mabega.

Jamaa alishindwa kuendelea na mazungumzo, akaacha kinywaji chake na kwenda kukilipia.

Baada ya kulipa bili yake, aliondoka upesi, akapanda pikipiki na kwenda zake kukutana na marafiki.

Alipowasimulia kilichompata, walimwambia alifanya vyema kujitoa kwenye meno ya simba.

Kalameni mmoja alidai alijipata katika hali sawa alipokutana nakipusa mara ya kwanza baada ya kurushiana misitari mtandaoni.

“Huyo ni slay queen. Umefanya vizuri kuhepa. Vipusa kama hao wanaweza kukufanya ulale seli za polisi. Hawa warembo weupeweupe wana majaribu mengi,’’ kalameni alisema.

Polo huyo aliapa kwamba hatasaka warembo kwenye mitandao ya kijamii tena kufuatia kioja hicho.

…WAZO BONZO…

You can share this post!

Ford Kenya na ANC wakosa kuafikiana

Sukari ya Sh5 bilioni kusalia bandarini

adminleo