Dondoo

Kioja keki ikikataa kukatika katika harusi sababu ya deni

Na BENSON MATHEKA April 21st, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KITOTO, Makueni:

KIOJA kilishuhudiwa katika harusi moja hapa keki ilipokataa kukatika hadi mwenye kuipika alipolipwa deni lake.

Inasemekana kila kitu kilionekana kuenda sawa hadi wakati wa kukata keki ulipofika.

Bw Harusi na Bi Harusi walisonga mbele ya wageni kuikata na kuinua kisu kwa bashasha.

Hata hivyo, walipojaribu kukata keki, haikukubali kabisa! Walijaribu mara kadhaa bila mafanikio, huku wageni wakishangaa.

Ilibainika kuwa mpishi hakuwa amelipwa alivyokuwa amekubaliana na maharusi na alitumia mazingaombwe yake.

Baadaye alitumiwa pesa kwa simu huku emcee akifanyia mzaha tukio hilo kuficha ukweli kisha kesi ikakubali kukatika kwa urahisi sana.