• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Jiji la Nairobi lingali chafu chini ya usimamizi mpya

Jiji la Nairobi lingali chafu chini ya usimamizi mpya

Na CHARLES WASONGA

ATHARI za hatua ya majuzi ya Gavana wa Kaunti ya Nairobi Mike Sonko kudinda kuidhinisha mgao wa Sh15 bilioni kwa Nairobi Metropolitan Services (NMS) zimeanza kuoneka kutokana na uchafu uliokithiri katikati mwa jiji.

Katika uchunguzi wetu katika barabara kadha za katikati mwa jijini la Nairobi jana, mandhari iliyotualika ni ya marundo ya taka katika barabara zenye shughuli haswa mitaa ya downtown town.

Na katika barabara mpya ya Luthuli ambayo ilipanuliwa na kuboreshwa mwaka jana kwa kima cha Sh236 milioni mapipa ya taka yalikuwa yamejaa pomoni. Takataka zilikuwa zimetapakaa kote katika barabara hiyo ya unaongana na River road (upande wa chini) na Tom Mboya Street (upande wa juu).

Hali hivyo hivyo katika barabara ya Kirinyaga Roas ambapo wafanyabiashara wengine wanalalamikia marundo ya takataka ambayo yametapakaa nje ya malango ya maduka yao.

Waziri wa Mazingira Larry Wambua hakujibu simu zetu wala ujumbe mfupi tulipotaka kufahamu ni kwa nini taka zimetapaka katikati mwa jiji haswa wakati huu wa janga la corona ambapo usafi ni muhimu.

Hata hivyo, afisa mmoja wa kaunti ambaye aliomba tusimtaje jina kwa sababu haruhusiwi kuongea na wanahabari alisema hali hiyo inachangiwa na sababu kwamba wengi wa wafanyakazi wa kampuni za kibinafsi ambazo huzoa taka hawajalipwa malimbikizi ya mishahara.

“Hali hii ni uchafu katika barabara za jiji zitaendelea hadi pale wazoaji taka walioanza kugoma mwezi jana watalipwa. Hata hivyo, nasikia kuwa wala ambao hufagia katika maeneo ya Moi Avenue kwenda juu wamelipwa sehemu ya pesa wanazodai,” akasema.

Mwanzoni mwa mwezi wa Machi wazoaji taka walifanya mgomo uliodumu kwa wiki tatu wakidai malipo ya mishahara yao ya kuanza Januari mwaka huu.

Wafanyakazi hao wa kampuni za kibinafis walifanya maandamano katikati mwa barabara za jijini wakirusha taka katika barabara kote. Bw Wambua aliondoa lawama kwa idara yake akielekeza kidole cha lawama kwa idara ya Fedha kufuatia sintoifahamu ilisababisha na mgogoro miongoni mwa maafisa husika.

Katika bajeti ya ziada iliyopitishwa na Kamati ya Bajeti ya Bunge la Kaunti ya Nairobi idara ya uzoaji taka, ambayo ni miongoni mwa majukumu ambayo ilihamishwa hadi NMS ilitengewa Sh400 milioni. NMS inaongozwa na Meja Jenarali Mstaafu Mohammed Badi ambaye aliteuliwa na Rais Uhuru Kenyatta kuwa kushikilia wadhifa wa Mkurugenzi Mkuu (DG)

Pesa hizo ambazo ni sehemu ya Sh15 bilioni ambazo zilipasa kuendea NMS ndizo zilitarajiwa kulipa mishahara ya wazoaji taka katikati mwa jiji.

Lakini Bw Sonko alikataa kuidhinisha bajeti hiyo akidai ilijumuisha majukumu mengine ambayo sehemu yake haikuhamisha hadi Serikali Kuu.

You can share this post!

Rais ahakikishia taifa mitihani ya kitaifa itafanywa mwaka...

MaruFuku ya FIFA kuhusu Amrouche si mwisho wa dunia -FKF

adminleo