• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 6:39 PM
Kamishna atahadharisha viongozi dhidi ya siasa kuingizwa katika ujenzi wa bwawa

Kamishna atahadharisha viongozi dhidi ya siasa kuingizwa katika ujenzi wa bwawa

Na Kenya News Agency

KAMISHNA wa Kaunti ya Kirinyaga Birik Mohammed amehimiza viongozi kutoingiza siasa katika mradi wa Sh19 bilioni wa ujenzi wa bwawa la Thiba.

Bw Birik alisema siasa duni ikiwemo uchochezi wa watu fulani utachelewesha utekelezaji wa mradi huo unaostahili kuanza Machi.

Kamishna huyo alikuwa akizungumzia habari za maandamano ya wakazi katika eneo la Mutithi mjini Mwea ambako ofisi ya mradi imefunguliwa. Alisema manaibu kamishna wote wa kaunti hiyo wanahitajika kuongoza shughuli ya kusajili wafanyakazi watakaohudumu katika mradi huo wa ujenzi, utakaochukua miaka mitatu hadi minne.

“Ni msimamo wa serikali kwamba mradi huu wa bwawa utekelezwe bila ya kuingizwa siasa duni. Tutahakikisha manaibu wa makamishna wanashiriki kikamilifu,” akasema.

Awali, afisa katika Kitengo cha Utekelezaji Mradi alimfahamisha Bw Birik kwamba kati ya wakazi 60 waliohojiwa ili kuendesha mashine za uchimbaji, hakuna aliyefaulu.

You can share this post!

Msomi ataka ushirikiano Pwani

Watatu wafariki baada ya malori mawili kugongana na kushika...

adminleo