• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 7:47 PM
Kanisa Katoliki lapiga marufuku nguo za kubana mwili kanisani

Kanisa Katoliki lapiga marufuku nguo za kubana mwili kanisani

NA SAMMY KIMATU

KANISA Katoliki lililo jijini Nairobi limeshangaza wengi kwa kuchapisha na kutundika bango langoni kuhusu mavazi ambayo hayastahili kuvaliwa kanisani.

Bango hilo kubwa katika lango la Kanisa Katoliki la St Peter Clavers lilio katikati mwa jiji, limechapisha picha za mavazi kama vile zilizopasuliwa na kuonyesha mapaja, minisketi na blauzi zilizowacha kifua wazi.

Nguo zingine ni suruali ndefu zinazoacha sehemu za mwili wazi baada ya kutobolewa mashimo miguuni, zile za kubana na pia miwani mieusi inayoficha uso, bangili na kofia.

Hili ni kanisa la pili jijini Nairobi kutangazia hadharani waumini mavazi ambayo hayaambatani na maadili ya kanisa baada ya lile la Askofu James Ng’ang’a wa Neno Evangelism Centre.

Juhudi zetu kutaka kuwahoji wasimamizi wa kanisa hilo hazikufua dafu kwani hawakupatikana. Hata hivyo, waumini na wananchi wengine walitoa hisia mseto kuhusu hatua hiyo.

Bw Alex Muinde, 26, alisema kuna uhuru wa watu kuvalia kulingana na chaguo lao binafsi na kanisa haliwezi kuonyesha mtu nguo ile atavaa na asistahili kuvaa.

Lakini Bw Peter Kuria, 52, mfanyabiashara alisema siku hizi wanawake huvalia vibaya na inastahili wapewe mwongozo.

Na Sammy Kimatu?”Nguo hizi huwa zinanafa fikra za wanaume wakati wa ibada makanisani,” Bw Kuria asema.

Dereva wa matatu nambari 33 za kwenda Ngumo/Mjini Bw Joseph Omollo, 65, aliunga mkono watu kukatazwa kuvalia mavazi hayo akidai wazazi ndio wa kulaumiwa pakubwa kwa kikosa kuonyesha binti zao jinsi ya kuvaa.

“Serikali iingilie kati kwa sababu wazazi wameshindwa kudhibiti tabia na maadili ya watu,” Bw Omollo akasema.

Binti Rosalia Alexis, 29 aliye mwanasayansi alikubaliana na kanisa akisema wanaume wana hisia za kuvutiwa na wanawake wakivalia vibaya.? “Nguo sampuli hii ni za kuvaliwa katika kumbi za densi na disko wala sio kanisani,” akasema.

Mfanyakazi wa benki, Bw Sosmas Moula, 53 asema makanisa yamechelewa kutoa ilani hii mapema na kulinganisha na wanawake wasiofunga vitambaa vichwani kuwa ni makosa.

Bi Hilda otieno, 44, mshauri wa masuala ya fedha asema matangazo kwenye runinga na wasanii wa nyimbo ndio wa kulaumiwa pakubwa kwa kuvalia mavazi mambaya na kushauri kwamba watoto waelekezwa jinsi ya kuvaa na wazazi wao.

Kwa Bi Rosemary Nzyoki, 38 anasema ata mwilini aina ya Tatoo kando na mavazi haya ni janga lililokita mizizi miongoni mwa vijana wetu.

“Biblia inatufunza watoto kuwa watiifu lakini siku hizi huwezi kumrekebisha au kumkosoa mtoto asiye wako kwa kuhofia kushtakiwa kwa machifu,” Bi Rosemary akaambia Taifa Leo.

You can share this post!

Waiguru amezea mate cheo cha juu

Wasafiri waumia mabasi ya Modern Coast yakizimwa

adminleo