• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 8:55 PM
Mkurugenzi aliyejiuzulu kusalia ofisini kwa miezi 6

Mkurugenzi aliyejiuzulu kusalia ofisini kwa miezi 6

Na BERNARDINE MUTANU 

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Family David Thuku amejiuzulu.  Kulingana na taarifa JumanneDkt Thuku alijiuzulu kwa lengo la kutekeleza maazimio ya kibinafsi. 

Alihudumu kwenye benki hiyo kwa muda wa miaka mitano na nusu kabla ya kuchukua uamuzi huo. 

Lakini atasalia ofisini kwa muda wa miezi sitampaka benki hiyo ipate afisa atakayechukua mahali pake. 

Alipata wadhifa wa mkurugenzi mkuu April 2016 baada ya kuondoka kwa Bw Peter Munyiri. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Family Bank Wilfred Kiboro alimshukuru kwa kazi yake shwari kwani ni kupitia kwa usimamizi wake ambapo benki hiyo ilikuwa imeanza kupata faida tena. 

Tunamtakia kila lema katika anachoenda kufanya,” alisema Bw Kiboro kwa niaba ya bodi hiyo. 

You can share this post!

Sukari yote yenye nembo ya Mumias ni feki – Ripoti

Mtakiona mkipandisha bei ya unga, serikali yaonya...

adminleo