• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Polisi auawa na wanakijiji baada ya kumuua mkewe

Polisi auawa na wanakijiji baada ya kumuua mkewe

Na SAMMY LUTTA

AFISA wa polisi aliuawa na umati muda mfupi baada ya kudaiwa kumuua mkewe katika kijiji cha Lokangai, Kaunti Ndogo ya Turkana Magharibi.

Wakazi walimkamata Andrew Etabo, 40 alipojaribu kutoroka baada ya kumuua mkewe Pauline Longole, 20.

Mkuu wa polisi wa eneo hilo, Bw Joseph Cheruiyot alisema afisa huyo alitumia kipande cha mti kumuua mkewe.

“Mwanamume huyo alipokuwa akitoroka, majirani waliokuwa na hasira na wakazi wengine walimkamata na kumuua kwa kumpiga mawe,” alisema Bw Cheruiyot.

Afisa huyo alisema mwanamke huyo alifariki baada ya kuvuja damu nyingi. Wawili hao wameacha mtoto mwenye umri wa miaka minne.

Bw Cheruiyot alisema polisi wameanza uchunguzi kubaini kilichosababisha ugomvi uliofanya mwanamume huyo kumuua mkewe.

Aliwaonya wakazi kutochukua sheria mikononi akisema wanapaswa kuwapeleka washukiwa kwa polisi.

Kisa hiki kilijiri wiki moja baada ya kingine ambapo umati ulimuua dereva wa kampuni ya China Road Construction Company.

  • Tags

You can share this post!

Wanaodaiwa kuua binti wa hakimu kujibu mashtaka Ijumaa

Wanakijiji 300 wakesha kwa kijibaridi kufuatia mzozo wa...

adminleo