Kilio kuhusu gharama kubwa ya lishe ya ng’ombe wa maziwa nchini
KUPANDA kwa bei ya lishe, umeme na vifaa muhimu kumetajwa kama tishio kwa ukuaji wa sekta ya ufugaji ng’ombe wa maziwa nchini.
Kulingana na Bodi ya Maziwa Kenya (KDB), gharama ya uzalishaji wa lita moja ya maziwa ni kati ya Sh30 na Sh37, kutegemea mfumo wa ufugaji na kiwango cha uzalishaji.
Wafugaji ng’ombe wa maziwa nao wanasisitiza kuwa ongezeko la bei ya lishe linasalia kuwa changamoto kuu, haswa kwa wale ambao wanaendesha mfumo wa ufugaji ambapo ng’ombe huwaachwi kurandaranda kusaka lishe bali hununuliwa lishe.
Hata hivyo, data kutoka kwa KDB inaonyesha kuwa Kenya inasalia kuwa mojawapo ya mataifa yanayoongoza katika uzalishaji wa maziwa na bidhaa husika, ikiorodheshwa ya pili nyuma ya Misri.