Habari Mseto

Huzuni mkulima akifariki baada ya kuangukiwa na mpapai

Na CHARLES WANYORO August 9th, 2024 1 min read

WAKAZI wa kijiji cha Kiraro, Maara, Kaunti ya Tharaka Nithi wanaomboleza kifo cha mkulima mmoja alipoangukiwa na mpapai.

Bw Kimathi Mbaya alishinda Alhamisi akipanda migomba na kazi nyingine shambani na baadaye akaamua kuchuna papai lililoiva ajali ilipotokea mpapai huo ulipomwangukia akafariki papo hapo.

Jirani yake, Bw Eliaza Kamundi alisema alisikia nduru kutoka kwa wapita njia na alipoenda kujua kilichojiri akapata mkulima huyo akiwa ameangukiwa na mpapai.

Alisema walikimbia alipokuwa mkulima huyo na kuondoa mti kumuokoa lakini wakagundua alikuwa amekufa.

Bw  Kamundi alisema huenda alisikia sauti ya mti ukianguka lakini hakufuatilia sana kwa kuwa kulikuwa na shughuli nyingi eneo hilo.

“Nilikuwa nikichoma mahindi niliposikia kitu kikianguka lakini nikachukulia ilikuwa tawi la mti aliokuwa akikata lilioanguka. Ni baada ya baadhi ya vijana kunipasha kuhusu mkasa huo nilipogundua kilichofanyika,” alieleza.

Wakazi walikusanyika eneo la mkasa wakiwa wameshtuka.

Mkazi mwingine, Kinyua Nabea alimtaja mkulima huyo kama mwanaume aliyekuwa na bidii ambaye alikuwa akishinda shambani au katika shughuli zake.

  • Tafsiri: Benson Matheka