Habari za Kaunti

Mama, mpenziwe wazuiliwa kwa mauaji ya watoto

Na ERIC MATARA July 22nd, 2024 1 min read

POLISI wanaendelea kumzuilia mama mmoja na mpeziwe katika kituo cha polisi cha Litein, Kaunti ya Kericho, baada ya kuwaua watoto wawili wenye umri wa miaka sita na minane.

Tukio hilo lilifanyika mnamo Julai 12, katika kijiji cha Sibaik, eneobunge la Bureti. Maafisa wa upelelezi walimkamata Bi Brenda Cheptoo, wiki moja baada ya watoto hao kupatikana wakiwa wamefunikwa na blanketi kwenye kaburi wiki iliyopita.

Afisa wa upelelezi alisema mshukiwa huyo alikiri kuwaua wanawe kwa sumu kabla ya kuwazika akiwa na tumaini la kuolewa.

“Alikamatwa katika eneo la Litein pamoja na mpeziwe. Bi Cheptoo alikiri kuwaua akiwa na azma ya kusalia huru ili aolewe.”