Habari za Kitaifa

Polisi walemewa Karatina huku waandamanaji wakijaribu kuvunja Benki ya Equity


KARATINA 3.50 PM

MAMIA ya waandamanaji ‘wameteka’ mji wa Karatina, katika Kaunti ya Nyeri baada ya kuzidia nguvu maafisa wa polisi waliolazimika kuondoka.

Makundi hayo ambayo yamezua ghasia yamefunga barabara kuu ya Karatina-Nairobi na kutatiza shughuli za uchukuzi kwenye barabara hiyo yenye shughuli nyingi.

Kufikia wakati wa kuandika ripoti hii, hakukuwa na dalili yoyote ya polisi licha ya kwamba baadhi ya waandamanaji walijaribu kuvunja ili kuingia afisi ya Benki ya Equity kabla ya walinzi kufunga benki hiyo mara moja.