Habari za Kitaifa

Polisi waliojihami wawasili upesi kulinda jengo la Mandago

Na TITUS OMINDE July 16th, 2024 1 min read

POLISI waliojihami wamewasili haraka kulinda jengo la Liaison Office linalohusishwa na Seneta wa Uasin Gishu Jackson Mandago katika mtaa wa Elgon View, Eldoret kufuatia ripoti kwamba vijana walikuwa wanapanga kuivamia.

Ripoti zinasema fununu zilienea kwamba kulikuwa na kundi la vijana wa Gen Z waliokuwa wanapanga kuvamia ofisi hiyo kwa sababu ya kashfa ya elimu Finland ambayo Seneta huyo anadaiwa kupokea mamilioni ya pesa kutoka kwa wazazi na kukosa kutimiza ahadi hiyo.

Zaidi ya polisi 10 waliojihami vikali walipiga kambi; ingawa vijana hawakutimiza vitisho vyao kufuatia mgawanyiko kuibuka baina yao.

Maandamano hayajachacha mjini Eldoret huku wachache waliojitokeza wakikamatwa upesi na kufungiwa na polisi.