Habari

Red Cross yaomba msaada wa Sh1 bilioni kukabili njaa nchini

February 22nd, 2018 1 min read

Na BERNARDINE MUTANU

Mabadiliko ya hali ya anga yameonekana nchini kwa muda ambapo kila mwaka wananchi wameonekana kuhitaji chakula.

Hivi sasa, wananchi kufikia milioni 3.4 wanahitaji msaada wa chakula katika kaunti kame nchini. Kati yake, wananchi 1.4 milioni wanahitaji msaada huo kwa dharura.

Shirika la Msalaba Mwekundu Februari 22, 2018 limezindua ombi jipya la ufadhili kutoka kwa wananchi.

Ili kuweza kukabiliana na hali hiyo katika Kaunti za Garissa, Wajir, Isiolo, Tana River, Kajiado na Kilifi, shirika hilo linahitaji ufadhili wa Sh1 bilioni.

Kaunti zingine ambazo zinafuatiliwa kwa karibu ni Mandera, Marsabit, Kitui na Taita Taveta.

Habari zaidi kufuata…

Video Gallery