NA MASHIRIKA
PARIS, UFARANSA
RAIS Emmanuel Macron wa Ufaransa ataanza kuhudumu kwa kipindi cha pili kama rais, baada ya kutangazwa mshindi kwenye duru ya pili ya uchaguzi wa urais uliofanyika Jumapili.
Macron aliibuka mshindi kwa kuzoa asilimia 58.6 ya kura dhidi ya Marine Le Pen.
Wafuasi wake walishangilia ushindi huo kwenye barabara za jiji kuu, Paris, kati ya miji mingine.
Kwenye hotuba yake ya ushindi, aliahidi kurejesha tena hali ya mshikamano nchini humo.