• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Mademu, hakikisheni mnazaa na wanaume walio na akili, Jackie Matubia ashauri

Mademu, hakikisheni mnazaa na wanaume walio na akili, Jackie Matubia ashauri

NA FRIDAH OKACHI

Mwigizaji Jackie Matubia amesimulia mahangaiko ya kulea wanawe wawili bila kupata usaidizi wa baba zao.

Bi Matubia ni mama wa watoto wawili wa kike, na mwigizaji kwenye kipindi cha Salem na pia aliigiza katika vipindi vya  Zora na Tahidi High.

Kwenye chaneli yake ya YouTube, Matubia alizungumzia kwa undani kilichomfanya kukatiza uhusiano wake na mwigizaji Blessing Lung’aho waliyekutana kwenye kipindi cha Zora.

Mwigizaji huyo amewataka wanawake kutafuta mahusiano na watu walio na akili, akimsifia baba wa mwanawe kifungua mimba.

“Zaeni na watu walio na akili…..mwanangu alisema nataka kusafiri, niliamua kutimiza hilo na babake alisaidia kwa jukumu hilo, kiliniramba” alisema mama huyo.

“Hata mimi kiliniramba, lakini uzuri wangu napenda kuwa mkweli, na kuzungumza ukweli jinsi ulivyo, maana ndilo jambo ambalo hunipa furaha,” aliendelea.

Mama huyo alisema Blessing Lung’aho ambaye ni baba wa mtoto wa pili, hajakuwa akimsaidia kulea hata baada ya kuachana miezi michache iliyopita.

Matubia alisisitiza kwamba maisha yake tangu kuachana na Lung’aho hayajakuwa rahisi na kwamba ni Mungu tu amekuwa akimshikilia muda wote.

Mungu kwa kweli amekuwa katika kitovu cha maisha yetu, mimi na mabinti zangu, amenishikilia sana wakati kila kitu katika maisha yangu kilikuwa kinasambaratika. Mungu alinishika mkono na kunipa nguvu za kuwa mama na baba wa watoto wangu,” Matubia alisema.

“Lakini nitasema hivi unapoteza kitu kimoja unapata vingi,” aliongezea.

Kwenye video hiyo Matubia amewataka wanawake kujipenda na kukosa kupeana kila kitu alicho nacho.

“Kila wakati nimekuwa napeana, kupeana hadi unajisahau,” alisema Matubia.

Matubia na Lung’aho waliachana miezi kadhaa iliyopita kila mmoja akinyamaziana na kukosa kujitokeza na kuzungumza kama wako pamoja au la.

Baada ya uvumi kuenea wawili hao wameachana, Lung’ano alihojiwa na Presenter Ali na kudai kuwa wote wako sawa na hakuna jambo hilo.

  • Tags

You can share this post!

Uhuru alihepwa na kuaibishwa na Wazungu aliposhtakiwa...

Mkuu wa Bandari Lamu atoa sababu ya meli ya watalii kufunga...

T L