• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 11:55 AM
Mdalasini na faida zake mwilini

Mdalasini na faida zake mwilini

NA MARGARET MAINA

[email protected]

MBALI na faida za kiafya ambazo mdalasini hutoa, ni muhimu pia katika masuala ya urembo.

Mdalasini huongezwa katika vyakula kwa sababu huongeza ladha kwa chakula.

Mdalasini huwa na virutubisho vingi. Huwa na madini kama vile potasiamu, manganese, kalsiamu, magnesiamu, zinki na chuma.

Virutubisho hivi husaidia kupunguza shinikizo la damu na viwango vya sukari kwenye damu. Pia hutibu shida za wanawake, magonjwa ya kupumua na shida za kumeng’enya chakula.

Maji ya mdalasini

Maji ya mdalasini pamoja na asali ni kinywaji bora kwa wanaotaka kupunguza uzani, kwani yanasaidia kuondoa sumu mwilini. Maji ya mdalasini hukufanya ujisikie umeshiba na kuzuia njaa na hamu ya chakula. Hii inasaidia kupoteza uzito haraka.

Wanawake ambao wana maumivu ya wakati wa hedhi wanaweza kunywa maji ya mdalasini ambayo husaidia kupunguza maumivu hayo. Mdalasini huwa na analgesic na anti-coagulate ambayo husaidia kupunguza maumivu.

Huongeza kinga

Maji ya mdalasini yana antioxidants kama polyphenols na proanthocyanidins ambazo husaidia kuimarisha mfumo wa kingamwili. Pia, maji ya mdalasini yana anti-fungal, antibacterial na antiviral na hivyo hupunguza magonjwa kama shida za moyo, magonjwa ya kupumua, na kadhalika.

Huboresha namna ubongo unavyofanya kazi

Maji ya mdalasini huboresha kumbukumbu na kukuza utendaji wa ubongo. Mdalasini huwa na uwezo wa kupunguza kasi ya ukuaji wa magonjwa ya ubongo kama ugonjwa wa Parkinson na Alzheimer’s. Maji ya mdalasini pia husaidia katika kuimarisha utulivu na umakini.

Hupunguza maumivu ya meno

Mara nyingi tunasumbuliwa na maumivu ya meno ambayo hayavumiliki. Mdalasini ni kiungo chenye nguvu na huwa na uwezo wa kuponya jino linalouma. Kunywa maji ya mdalasini kutapunguza maumivu ya meno na pia kutapunguza uvimbe wa ufizi.

Huboresha ngozi

Maji ya mdalasini husaidia katika kuboresha ngozi. Mdalasini ni chanzo bora cha nyuzi ambazo husaidia kuondoa sumu kutoka kwa mwili.

Hii inazuia sumu zenye mazoea ya kutoka na kuziba ngozi.

  • Tags

You can share this post!

Mahakama ya juu yaombwa iruhusu mpango wa BBI wa...

Mwanasoka anayelenga kufuata nyayo za Sergio Ramos wa PSG

T L