Na SHABAN MAKOKHA
MBUNGE wa Mumias Mashariki Benjamin Washiali, ambaye alitangaza kuwa hatatetea kiti chake, amempendekeza mwalimu kama mrithi wake kabla ya Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9.
Bw Benson Mapwoni Makokha, sasa atapeperusha bendera ya United Democratic Alliance (UDA) katika eneobunge hilo.
Anatarajiwa kumenyana Mabw David Wamatsi, Peter Salasya, Kassim Were, Lucas Radoli na Paul Makokha wanaomezea kiti hicho.
“Nawashukuru watu wa Mumias kwa sababu baada ya kunichagua niwawakilishe bungeni kama mbunge wao, niliteuliwa kuhudumu kama naibu kiranja mkuu kwa miaka mitano na hatimaye kama kiranja mkuu,” alisema Bw Washiali anayehudumu kwa muhula wake wa tatu.