• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Bei ya stima haitapanda kwa sababu ya ushuru mpya

Bei ya stima haitapanda kwa sababu ya ushuru mpya

Na BERNARDINE MUTANU 

Gharama ya stima haitapanda kutokana na ongezeko la bei ya mafuta. Ongezeko la bei ya mafuta lilianza kutekelezwa Septemba 1, baada ya sheria ya asilimia 16 ya VAT kwa bidhaa za mafuta kuanza kutekelezwa. 

Kulingana na Katibu Mkuu katika Wizara ya Kawi Joseph Njoroge, kuzinduliwa kwa kiwanda cha megawati 310 Turkana kutasaidia kukabiliana na ongezeko la gharama ya matumizi ya stima.

“Kwa sababu ya kawi ya upepo, kiwango cha dizeli kitakachotumika kuzalisha kawi kitakuwa cha chini kiasi kwamba watumiaji wa stima hawatahisi hiyo asilimia 16 VAT,” alisema katibu huyo.

Alikuwa akijibu maswali yaliyoibuliwa na kamati ya kawi katika Seneti kuhusiana na athari za ushuru huo kwa gharama ya stima.

Kwa sasa, stima inayozalishwa kwa kutumia dizeli ni ghali.

You can share this post!

Serikali kuongeza ada ya NHIF

Familia tajiri hazijadai Sh10.5b zilizoachwa na wapendwa...

adminleo