• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 8:27 PM
Pasta azaba kidosho kofi kwa kumtongoza

Pasta azaba kidosho kofi kwa kumtongoza

Na JOHN MUSYOKI

Machakos

KIPUSA mmoja kutoka mahali hapa alikiona cha mtema kuni alipozabwa makofi na pasta kwa kumtongoza walipokutana njiani.?

Inasemekana pasta na demu huyo walikuwa marafiki hapo awali lakini wakakosana baada ya jamaa kuamua kumtumikia Mungu.

Baada ya pasta kumaliza masomo yake ya innjili, aliendelea kuhubiri akiwa katika harakati za kutafuta mwanamke wa kuoa.? Siku ya kioja, pasta alipokuwa akielekea nyumbani kutoka kanisani, alikutana na mpenzi wake wa awali.

Demu alianza kueleza jinsi alivyokuwa akimpenda pasta huyo na kumlaumu kwa kumpuuza.

“Hei, nimekuwa nikikutafuta kwa muda mrefu. Mimi bado ninakupenda. Najua unaendelea kutafuta mwanamke wa kuoa. Kumbuka tulianza uhusiano wetu kitambo na hakuna haja ya kuhangaika nikiwa hapa. Niko sawa,” demu alimwambia pasta.

Pasta kwa upande wake alimpuuza lakini demu bado alisisitiza kwamba alikuwa anampenda.

“Hata hauna haya kusimama mbele yangu na kuanza kunihadithia stori kama hizo. Mimi sitaki hadithi zako. Kumbuka vile ulivyonitesa na kuniona nikiwa mtu bure kabisa. Nilipoamua kuwa pasta uliniacha na kunirushia cheche za matusi. Ulikuwa unataka nifanye nini? Baadaye ulianza kutembea na wanaume mitaani. Wewe ni kahaba. Toka mbele yangu kabla sijachemka,” pasta alimwambia kipusa.

Licha ya demu kukemewa na pasta, alisisitiza kwamba mtumishi wa Mungu alikuwa wake.

“Wewe ni wangu na mtu akijaribu kuja kujipendekeza kwako nitapambana naye kufa kupona,” demu alimwambia pasta.? Pasta alikasirika na kumwangushia demu kofi moto la usoni.

“Wacha kunisumbua. Sitaki presha zako. Hata ukijipendekeza kwangu mimi siwezi kukuoa. Kwenda kabisa,” pasta alifoka.

Inasemekana baada ya demu kuangushiwa kichapo, alitoka shoti mfano wa mtu aliyefukuzwa na mapepo na kutoweka asijulikane ameenda wapi.

 

You can share this post!

Kusafiri Kisumu kwa ndege sasa ni ghali kuliko Mombasa

Kundi sasa lapinga Disney kumiliki “Hakuna Matata”

adminleo