Afya na Jamii

Wanaume huchoma kalori zaidi kuliko wanawake wakishiriki mchezo wa huba -Watafiti

Na CECIL ODONGO August 6th, 2024 1 min read

WANAUME huchoma zaidi mafuta mwilini wakati wa tendo la ndoa kuliko wanawake, watafiti wamebaini.

Kando na raha inayotokana na kujamiiana, wanaume huchoma mafuta mengi wakijizatiti kuwaridhisha wapenzi wao wakati wa huba.

Utafiti huo ulionyesha wanaume huchoma kalori 101 wakati wa mapenzi huku wanawake wakichoma kalori 69 pekee.

Kwa mujibu wa Mtaalamu wa Afya, Leah Millheiser, wanaume ndio mara nyingi hujizatiti sana kitandani wakati wa kitendo cha kujamiiana.

Kujizatiti kwao kunaweza kufasiriwa au kulinganishwa na kufanya mazoezi ndiposa wao hunufaikia kuchoma mafuta mwilini.

“Kuna tofauti kati ya tendo la ndoa ambalo huchukua dakika tano lakini ni la kasi ya juu kuliko ile ambayo hudumu kwa saa kadhaa. Kila mtu huwa na hali tofauti kuhusiana na hili,” akasema mtaalamu mwengine Emily Morse kwenye mahojiano yaliyonakiliwa na jarida la The Newyork Post.

Hata hivyo, iwapo tendo la ndoa linaweza kufasiriwa kama mazoezi au kazi hutegemea mambo kadhaa.

Kati ya masuala hayo ni mtindo, muda na mahali ambapo mume na mke au wapenzi wanajaamiana.

“Iwapo unataka kudumu sana kitandani na kuchoma mafuta kupitia kutokwa jasho jingi, basi ni vyema iwapo wapenzi watakuwa wakijaribu mitindo mipya ya kufanya ngono,” akasema mtaalamu wa masuala ya mapenzo Jaimee Bell.

Hata hivyo, mafuta yanayochomwa mwilini wakati wa ngono ni madogo ikilinganishwa na yale ambayo yangemalizwa mwilini wakati wa mazoezi ya kawaida.

“Kando na kuongeza kasi ya kupumua, mpigo wa moyo na shinikizo la damu wakati wa kushiriki ngono, inaonekana kufanya mapenzi hakuwezi kuchukuliwa kama sehemu ya mazoezi. Hii ni kwa sababu manufaa yake ni madogo yakilinganishwa na kukimbia, kuendesha baiskeli na kuinua uzani,” akasema Mwanasayansi Dkt Jason Karp.