Habari za Kitaifa

Gachagua apata pigo korti ikiamua majaji hawakukosea kuketi Jumamosi kusikiza kesi ya Serikali

October 23rd, 2024 Kusoma ni dakika: 1

NAIBU Rais aliyetimuliwa mamlakani Rigathi Gachagua Alhamisi alipata pigo majaji watatu wa Mahakama Kuu walipoamua kuwa Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu hakukosea kuwateua kusikiliza kesi ya Bunge la Kitaifa na Mwanasheria Mkuu ya kutaka uamuzi wa kuzima kuapishwa kwa mrithi wake ifutwe.

Mnamo Jumanne, mawakili wa Bw Gachagua na wale wa washirika wake walipinga vikali jopo lililoteuliwa na Naibu Jaji Mkuu Mwilu wakisema alikuwa ametwaa mamlaka ya Jaji Mkuu Martha Koome na kwamba waliketi siku ya Jumamosi kusikiliza kesi ya kutaka uamuzi wa majaji wengine wawili wa kuzuia naibu rais mteule Kithure Kindiki kuapishwa.

Habari zaidi ni kadiri tunavyozipokea…