• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 9:55 AM
Lindeni watoto dhidi ya hatari za intaneti – Safaricom

Lindeni watoto dhidi ya hatari za intaneti – Safaricom

Na BERNARDINE MUTANU

Kampuni ya Mawasiliano ya Simu ya Safaricom imewashauri washikadau kuwalinda watoto dhidi ya hatari inayotokana na matumizi ya intaneti.

Afisa wa uhusiano wa wateja wa Safaricom Bw Stephen Chege alisema kampuni hiyo zaidi ya kulenga kuimarika kibiashara, inalenga pia kuimarisha usalama wa wateja wake hasa watoto.

“Tunataka kila mtu kuwa na uwezo wa kusoma mambo mapya bila kutishiwa usalama wao,” alisema Bw Chege.

Aliwataka wateja wa Safaricom kutumia intaneti kwa kuwajibika na kuheshimu watu wengine.

Mnamo Novemba 2018, Safaricom ilitia saini mkataba wa kuimarisha usalama katika matumizi ya intaneti pamoja na kampuni zingine za simu nchini.

Safaricom pia ilizindua sera ya kuwalinda watoto mitandaoni na inashirikiana na Wakfu wa Internet Watch Foundation kuziba maudhui ya ngono kwa watoto wake katika mfumo wake wa intaneti.

You can share this post!

Serena Hotels yafungua tawi jipya DRC

Raha kwa madereva wa Uber kupunguziwa bei ya mafuta

adminleo