Gavana akana uvumi kuhusu hali yake ya afya
GAVANA wa Taita Taveta, Bw Andrew Mwadime, amewasihi wanasiasa kukoma kueneza uvumi kuhusu hali yake ya afya.
Bw Mwadime alisema amekuwa akipokea matibabu baada ya kuhusika kwenye ajali Novemba 26, 2019 na kujeruhiwa kwenye utumbo.
“Wanasema nimekunywa pombe mpaka nashindwa kutembea. Hao ni wapinzani wameanza siasa, wacheni uchawi. Mwadime yupo sawa,” akasema.
Aliwaambia wakazi kuwa bado anaendelea na matibabu na yuko karibu kupona.
Wakati huo huo, Bunge la Kaunti ya Kilifi limeahidi kutilia maanani mapendekezo yaliyotolewa na umma kuhusu Makadirio ya Bajeti ya 2025/2026.
Hayo yamejiri huku Kamati ya Bajeti na Makadirio ikielekea faraghani kunakili ripoti ya mwisho na mapendekezo kuhusu bajeti hiyo, ambayo baadaye itawasilishwa katika Bunge la Kaunti ili ipitishwe.
Katika makadirio ya mwaka wa 2025/2026, Serikali ya Kaunti ya Kilifi imepanga kuweka kipaumbele kwa miradi ya afya, kilimo na maji katika bajeti ya mwaka huu.
Akiwasilisha mipango hiyo mbele ya Kamati ya Bunge la Kaunti, Waziri wa Fedha katika kaunti, Bi Yaye Shoshi, alisema juhudi zaidi zitaekwa ili kuboresha mapato ambayo kaunti hukusanya.
Kaunti hiyo imepanga kutumia karibu Sh19.6 bilioni mwaka huu, ambapo inatarajia kukusanya Sh1.9 bilioni kutoka kwa ada mbalimbali na huduma zinazotolewa na serikali ya kaunti.