SHANGAZI AKUJIBU Mke amekimya hata baada ya kugundua nina mpenzi wa kando, hii ni kawaida?
SWALI: Kwako shangazi. Mke wangu amegundua nina mpango wa kando baada ya kukagua simu yangu. Nimeungama na hajalalamika
Jibu: Siwezi kujua anachofikiria mke wako. Amejua kuwa ulimuacha ukaenda kutafuta mapenzi nje ya ndoa. Huenda ameamua kulipiza kisasi na ukijua hutakuwa na haki ya kumuuliza. Zungumza naye kabla mambo hayajaharibika. Ni kweli pia, kama ulivyosema, huwezi kujua anachopanga. Huenda anajaribu kuamua ikiwa ataendelea kukaa kwenye ndoa, aweke masharti mapya, au aondoke kabisa. Huenda pia anasubiri kuona hatua zako: kama una majuto ya kweli au ni maneno ya kuokoa hali tu.
IMETAYARISHWA NA WINNIE ONYANDO