Habari za Kaunti

Wanasiasa wa ODM wataka UDA isiwe na wagombea Mombasa

Na WINNIE ATIENO February 10th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

WANASIASA wa Chama cha ODM katika Kaunti ya Mombasa, wanashinikiza Chama cha UDA kikubali kutokuwa na wagombeaji kaunti hiyo.

Wakiongozwa na Diwani wa Wadi ya Shimanzi Priscilla Mumba, ambaye pia ni kiongozi wa walio wengi katika bunge la kaunti ya Mombasa, wanasiasa hao wamesema hawatakubali mchujo wa pamoja kati ya UDA na ODM.

Walisema UDA ikiweka makubaliano na ODM, inafaa kuiachilia kaunti ya Mombasa chini ya utawala wa chama cha ODM.