• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 12:48 PM
Mchungaji hali mahututi baada ya kuvamiwa na fisi

Mchungaji hali mahututi baada ya kuvamiwa na fisi

NA CHARLES WANYORO

MWANAUME mwenye umri wa miaka 54, kutoka Kaunti ya Marsabit, amelazwa katika hospitali ya Kenyatta akiwa katika hali mahututi, baada ya kuvamiwa na fisi mnamo Ijumaa.

Lepati Saidinga, alikumbana na mnyama huyo aliyemjeruhi kwenye meno na kuuma mboni ya jicho lake, punde tu alipokamilisha kuwapa mifugo wake maji na kuinama kunawa uso wake.

Fisi huyo pia aliuma vidole vyake vitatu kwenye mkono wake wa kulia, akajeruhi miguu yake na kumwacha na majeraha mabaya katika mkono wake wa kushoto. Kando na hayo, mnyama huyo wa mwituni alimng’oa meno mawili na kurarua jicho lake na pua.

Rafikiye, Lesapuk Namarti, 27, aliyefika kumwokoa, pia hakusazwa na fisi huyo alipomuuma kwenye mkono wa kushoto na miguu. Hata hivyo alipiga nduru na wachungaji wenzake wakafika kuwaowokoa kisha wakamuua mnyama huyo.

Msimamizi wa kitengo cha uuguzi katika hospitali ya Kenyatta, Yusuf Galmoge amesema Bw Saidinga alifikishwa humo akiwa hali mahututi na alifanyiwa upasuaji Jumamosi.

Bw Namarti naye amelazwa katika hospitali ya kaunti ndogo ya Laisamis, lakini madaktari hospitalini humo wamesema hayuko katika hali ya hatari.

You can share this post!

Mikono ya kijana aliyechomwa sababu ya ugali wa jirani...

Kaunti yataka Serikali Kuu ifungue kituo cha madini

adminleo