Makala

Je, wajua leo ni Siku ya Usingizi Duniani?

Na WINNIE ONYANDO March 13th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

HUKU dunia ikisherehekea Siku ya Usingizi Duniani wataalamu wanasema kuwa watu wanafaa kuhakikisha kuwa wanapata usingizi wa kutosha ili kuepuka maadhara yanayotokana na usingizi duni.

Kuendelea kukosa usingizi kumesababisha wasiwasi kwa wataalamu wa afya kwani kuna uhusiano kati ya usingizi duni na hatari ya magonjwa ya moyo, kisukari, unene kupita kiasi, na hata changamoto za akili kama vile msongo wa mawazo.

Takwimu za kitaifa zinaonyesha kuwa Wakenya wengi hawapati usingizi wa kutosha.

Kulingana na Sleep Diagnostic and Treatment Centre, takriban asilimia 40 ya wagonjwa wanapata tatizo la kupata usingizi (insomnia), asilimia 30 wanakabiliwa na sleep apnea, huku asilimia 15 wakikabiliwa na parasomnia, ikiwemo ndoto za kutisha usiku.

Vikas Patel, mtaalamu anayehusika na masuala ya mgongo kutoka Chuo Kikuu cha Colorado, Marekani, anaema kuwa ubora wa usingizi unategemea mazingira, hasa kitanda.

Kate Katisya, Meneja Mkuu wa Silentnight, alisema kuwa kupata usingizi wa kutosha ni muhimu kwa utendakazi wa mtu binafsi na kuwa afya ya familia.

“Kila mtu anapaswa kuhakikisha anapata usingizi wa kutosha ili kuendelea kuwa na nguvu,” alisema.

Kampuni hiyo pia imezindua aina mpya za vitanda vinavyolenga kuboresha usingizi, ikijumuisha teknolojia zinazodhibiti joto na kusaidia wale wenye matatizo ya mgongo.

Hii ni hatua inayolenga kusaidia Wakenya kupata usingizi bora, ambao ni msingi wa afya na ustawi wa familia.

Wataalamu wanashauri Wakenya kupanga muda wa usingizi, kuzingatia ubora wa vitanda na mazingira ya kulala, kwani usingizi mzuri ni silaha ya afya na ustawi wa maisha ya baadaye