Habari

MAFURIKO: Mmoja afa mvua kubwa ikianza maeneo mengi kama ilivyotabiriwa

Na KIMANI MWANGI March 21st, 2026 Kusoma ni dakika: 1

MVUA kubwa ilianza kunyesha Nairobi na sehemu zingine za nchi Ijumaa alasiri, ilivyotabiriwa na Idara ya Hali ya Hewa.
Tofauti na Ijumaa nyingine, mitaa ya jiji ilikuwa wazi zaidi kutokana na likizo ya Idd-ul-Fitr, inayoadhimisha mwisho wa mwezi mtukufu wa Ramadani. Mvua ilianza kunyesha jijini kuanzia saa tisa na dakika 20 alasiri.
Idara ya Utabiri wa Hewa iliwaonya wananchi wa kati ya nchi (pamoja na Nairobi), Bonde la Ziwa Victoria na Bonde la Ufa kuzingatia uwezekano wa mafuriko, barabara kuteleza na kuongezeka kwa maji ya mito.
Hali hiyo imesababisha kisa cha kifo Kilifi baada ya radi kupiga na upepo mkali kutokea katika Kaunti ya Kaloleni.
“Mwili umechukuliwa na kupelekwa mochari ya hospitali ya Mariakani huku watu wakitahadharishwa kuhusu hali mbaya ya hewa,” alisema Kamishna wa Kaunti, David Wanyonyi.
Mafuriko yaliripotiwa kaunti ya Narok na kuongezeka kwa udongo kwenye barabara ya Mai Mahiu–Suswa–Narok hasa eneo la Kedong.