Kimataifa

Wanaanga waliosafiri Mwezini warejea salama

Na MASHIRIKA April 11th, 2026 Kusoma ni dakika: 2

KIKOSI cha wanaanga wa Artemis II kilirejea salama duniani baada ya kukamilisha safari yao ya kihistoria mwezini.

Wanaanga hao wanne waliokuwa katika safari ya Artemis II ya NASA ya kuzunguka Mwezi baadaye walitua salama katika Bahari ya Pasifiki baada ya kurejea bila hitilafu yoyote.

Wafanyakazi hao sasa wako salama ndani ya meli iliyokuwa ikiwasubiri na wanaendelea kupumzika baada ya safari ya siku tisa iliyowapeleka mbali zaidi na dunia kuliko binadamu yeyote kuwahi kufika.

Chombo chao cha anga cha Orion kilikuwa kikisafiri kwa kasi ya zaidi ya maili 24,000 kwa saa (kilomita 38,600 kwa saa) na kilipoingia katika anga ya juu ya Dunia, ambapo ngao yake ya joto ilikumbana na halijoto inayokaribia nusu ya ile inayopatikana kwenye uso wa Jua.

Kurejea kwao wakiwa salama kunafungua njia kwa hatua inayofuata ya mpango wa Artemis, unaolenga kuwapeleka binadamu kwenye uso wa Mwezi na hatimaye kujenga makazi ya kudumu huko.

Joto kali lilisababisha chombo cha mawasiliano (Kapsuli) ambayo wanaanga waliipa jina la Integrity, kupoteza mawasiliano na kituo cha udhibiti wa misheni kilichoko Houston kwa dakika sita wakati wa kushuka.

Hata hivyo kulikuwepo na shangwe pale sauti ya Kamanda Reid Wiseman iliposikika akisema: “Houston, hapa Integrity. Tunawasikia vizuri kabisa.”

Hata hivyo kulikuwepo na hatari kubwa kwenye safari yao, muda mfupi baadaye miamvuli ya parachuti yenye rangi nyekundu na nyeupe ilifunguka na kuifanya chombo cha mawasiliano kushuka taratibu angani.

“Parachuti kuu ziko salama!” sauti ya maelezo ya NASA ilisikika mara kwa mara, hadi kapKsuli ilipotua baharini kwa mafanikio makubwa.

Wanaanga hao Wiseman, rubani Victor Glover, mtaalamu wa misheni Christina Koch, na mwanaanga wa Canada Jeremy Hansen walitolewa kwa uangalifu kutoka kwenye kapsuli na kusafirishwa kwa helikopta hadi kwenye meli ya USS John P Murtha, ambako watafanyiwa uchunguzi wa afya.

NASA ilisema watarejeshwa Houston ili kukutana tena na familia zao siku ya Jumamosi.

Walipokuwa wakisubiri kwenye sitaha ya meli, walionekana wakitabasamu na kuzungumza huku wakipiga picha.

Rais Donald Trump aliwakaribisha nyumbani na kusema safari yao ilikuwa “ya kuvutia sana,” huku akirudia mwaliko wa kuwataka watembelee Ikulu ya Amerika.
Hata hivyo, NASA bado haijathibitisha ni lini watajitokeza hadharani kwa mara ya kwanza.

Safari ya Artemis II ilianza hatua yake ya mwisho ya kushuka saa 19:33 EDT (23:33 GMT), wakati moduli ya huduma iliyotengenezwa na Wanaaga wa Yuropa (European Space Agency), sehemu yenye injini na paneli za nishati ya jua iliyoiendesha Orion katika safari yake ya Mwezi ilitenganishwa.