UDAKU: Tamaa ya visketi yamponza ‘paka mzee’ Romario kwa demu wake Tiffany
MWANASOKA nguli wa Brazil, Romario de Souza Faria, ameachwa na mpenzi wake kwa sababu ya kuwa na jicho kali la nje.
Jagina huyo, 60, alikuwa akichumbiana na Tiffany Barcelos — mwanafunzi anayetarajiwa kuwa daktari wa meno, ambaye pia ni mdogo wake miaka 35.
Romario anadaiwa kumwendea Tiffany kinyume na kuanza kutoka kimapenzi na Barbara Cavalcanti, ambaye ni rafiki mkubwa wa mrembo huyo.
Usaliti huo umeelezewa kuwa pigo kubwa kwa urafiki wa watatu hao kwani Barbara alikuwa msiri mkubwa wa Tiffany.
Hatua ya Tiffany inajiri baada ya Romario, ambaye ni mshindi wa Kombe la Dunia 1994, kuonekana katika eneo la watalii nchini Brazil akisisimuana kimapenzi na Barbara katika kundi la marafiki.
Tiffany ni mwanamke wa tatu kuhusishwa na Romario kimapenzi ndani ya kipindi cha miezi minne tu baada ya nguli huyo wa soka kukatiza uhusiano wake na mwanafunzi mwingine, Alica Gomes, 23.