Dondoo

Jombi achekwa kujidai simba baada ya kulewa pombe ya kudoea

Na BENSON MATHEKA May 12th, 2026 Kusoma ni dakika: 1

KWARE, Nairobi:

KICHEKO kilitanda katika mtaa mmoja baada ya lofa mmoja kujigeuza simba wa mtaa baada ya kulewa pombe aliyodoea kwa marafiki zake.

Jamaa huyo aliyekuwa ametembea siku nzima akiomba “ya kutoa lock,” alianza kupiga kelele na kujisifu kuwa hakuna mwanaume angeweza kumgusa.

Inasemekana baada ya kubugia chupa kadhaa bila kutoa hata senti moja, lofa alianza kuwasumbua watu kwa maneno ya kejeli huku akitembea kifua mbele kama tajiri.

Wakati mmoja alisimama katikati ya barabara akitangaza kuwa yeye ndiye “rais wa starehe” eneo hilo.

Hata hivyo, mambo yalibadilika ghafla alipojaribu kuzua fujo kwa vijana waliokuwa kijiweni.

Vijana hao walimkabili na kumtaka anyamaze au aondoke.

Simba huyo wa kulewa ya kuomba alitulia watu walipoanza kumcheka walipobaini alibugua pombe ya bwerere.