Kimataifa

Iran yaonya maadui wake wasithubutu kitu wanapomzika Ayatollah Khamenei

Na REUTERS July 3rd, 2026 Kusoma ni dakika: 1

TEHRAN, Iran:

KAMANDA wa Jeshi la Iran amezionya nchi za Amerika na Israel zisithubutu kushambulia taifa hilo linapojiandaa kuandaa mazishi ya kitaifa kwa Kiongozi wake wa Kidini Ayatollah Ali Khamenei.

Kiongozi huyo aliuawa mnamo Februari 28 wakati ambapo Amerika na Israel zilishambulia Iran kwa mara ya kwanza.

“Tunawaonya majirani wa Iran hasa Amerika na utawala wa Zayuni wa Israel zisithubutu kufikiria zitatushambulia. Majeshi yetu yamejiandaa vizuri kukabili hatari yoyote na zitajuta iwapo zitatuvamia,” akasema Kamanda Ali Abdollahi kupitia taarifa iliyosomwa na vyombo vya habari Iran.

Ali ndiye kamanda mkuu wa makao makuu ya jeshi ya Khatam al-Anbiya Central.

Msafara wa mazishi ya Khamenei utaanza Julai 4 jijini Tehran na kukamilika Julai 9 kisha atazikwa mji wake wa nyumbani wa Mashhad.

Pia kutakuwa na sherehe nyingine ambazo zimepangwa zitafanyika Qom na Iraq kati ya Julai 4 na Julai 9.

Mnamo Jumatano, Waziri wa Masuala ya Nje wa Iran Abbas Araqchi alitoa onyo kama hilo kwa Amerika na Israel.

Araqchi alisema kuwa wapo tayari kuyatekeleza mashambulizi makali zaidi kuhusiana na hatari zozote kwa watu na viongozi wa Iran.

Hii ni baada ya Waziri wa Ulinzi Israel Katz wa Israel kusema kwa kiongozi wa kisasa wa kidini ya Iran Mojtaba Khamenei anaandamwa ili auawe.

Iran imeimarisha hali ya usalama kuelekea na wakati huo wa msafara wa mazishi kwa kiongozi huyo wanayemrejelea kama shujaa.

Mkuu wa Shirika la Ndege Iran Jumatano alisema kuwa hakuna ndege ambayo itaruhusiwa kwenye anga ya nchi katika miji ya Tehran na Mashhad kama sehemu ya mikakati yake ya kiusalama.

Raia wengi wanatarajiwa kujitokeza kumuaga rasmi Khamenei.