Mwimbaji nguli Dolly Parton aombolezwa
MSANII maarufu wa ‘country music’, mtunzi wa nyimbo na mwigizaji wa raia wa Amerika Dolly Parton, alifariki Jumanne usiku akiwa na umri wa miaka 80.
Kifo chake kilithibitishwa na familia yake.
Parton alianza kuandika nyimbo akiwa na miaka sita. Wimbo wake wa kwanza, Little Tiny Tasseltop, ulihusu mwanasesere wake aliyependwa sana.
Nyimbo maarufu kama Jolene, Coat of Many Colors na I Will Always Love You, Parton aliziuza zaidi ya rekodi milioni 100 na kushinda tuzo 11 za Grammy, zikiwemo za heshima kwa mchango wake katika fani au tasnia ya muziki.
Alizaliwa Januari 19, 1946, Tennessee, katika familia maskini yenye watoto 12. Maisha yake magumu yalimchochea kuzama kwenye uimbaji na utunzi wa muziki.
Mbali na muziki, Parton alikuwa mwigizaji, mtangazaji na mfanyabiashara, akianzisha bustani maarufu ya Dollywood.
Pia alisaidia jamii kupitia programu za kusoma kwa watoto, ufadhili wa masomo na mchango wa dola milioni moja kwa utafiti wa chanjo ya Covid-19.
Parton alisema urithi wake mkubwa ungekuwa nyimbo alizoandika, akisisitiza: “Nyimbo ndizo urithi wangu.”